Select a date and time slot to book an Appointment
Date Of Appointment
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuwahimiza vijana kutokubali kushawishiwa kufanya vurugu na makundi ya watu wasiolitakia mema Taifa la Tanzania.


Badala yake, amewataka kuwa wazalendo na kulinda amani na utulivu wa nchi.
Dkt. Samia ameeleza kuwa Tanzania inaheshimika na mataifa ya nje kutokana na amani yake, na imekuwa kimbilio la watu wengi wanaokimbia machafuko katika nchi zao, hivyo amewahimiza vijana kuilinda heshima hiyo kwa kuhakikisha wanakwepa kuvuruga amani iliyopo.
Ametoa kauli hiyo katika kampeni zake kwenye Kata ya Runzewe, Wilaya ya Bukombe mkoani Geita leo Oktoba 12, 2025.
Kuhusu ahadi zake endapo atapata ridhaa ya wakazi hao, ni pamoja na ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu wa kisasa katika eneo la Ushirombo wilayani Bukombe.
Pia, amepanga kujenga skimu 10 za umwagiliaji maji katika wilaya hiyo ili kilimo kiweze kuwa biashara na kutengeneza fursa zaidi za kiuchumi na ajira kwa wakazi wa wilaya hiyo.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuwahimiza vijana kutokubali kushawishiwa kufanya vurugu na makundi ya watu wasiolitakia mema Taifa la Tanzania.
Badala yake, amewataka kuwa wazalendo na kulinda amani na utulivu wa nchi.
Dkt. Samia ameeleza kuwa Tanzania inaheshimika na mataifa ya nje kutokana na amani yake, na imekuwa kimbilio la watu wengi wanaokimbia machafuko katika nchi zao, hivyo amewahimiza vijana kuilinda heshima hiyo kwa kuhakikisha wanakwepa kuvuruga amani iliyopo.
Ametoa kauli hiyo katika kampeni zake kwenye Kata ya Runzewe, Wilaya ya Bukombe mkoani Geita leo Oktoba 12, 2025.
Kuhusu ahadi zake endapo atapata ridhaa ya wakazi hao, ni pamoja na ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu wa kisasa katika eneo la Ushirombo wilayani Bukombe.
Pia, amepanga kujenga skimu 10 za umwagiliaji maji katika wilaya hiyo ili kilimo kiweze kuwa biashara na kutengeneza fursa zaidi za kiuchumi na ajira kwa wakazi wa wilaya hiyo.



November 3rd 2025, 4:42 PM to December 6th 2025, 4:42 PM
We appreciate you contacting us. Our support will get back in touch with you soon!
Have a great day!
Please note that your query will be processed only if we find it relevant. Rest all requests will be ignored. If you need help with the website, please login to your dashboard and connect to support